Tunapopitia changamoto nyingi mara nyingi tunahangaika sana na wakati mwingine tukisahau kuwa yupo Mungu yeye muweza wa yote, yeye aponyaye na kutakasa, tabibu wa matabibu. Hakika majina yote mazuri ni yake. Hii ni baadhi ya mistari ya Biblia ya uponyaji, isome na ubarikiwe na kupokea uponyaji:- Isaya 40:29 Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo. Zaburi 147:3 Huwaponya waliopondeka moyo, na kuziganga jeraha zao. Isaya 57:18-19 Nimeziona njia zake, nami nitamponya, nitamwongoza pia, nitamrudishia faraja zake, yeye na hao wanaomlilia. Mimi nayaumba matunda ya midomo; Amani, amani kwake yeye aliye mbali, na kwake yeye aliye karibu; asema Bwana; nami nitamponya. Zaburi 103:2-5 Eeh nafsi yangu umhimidi Bwana, wala usizisahau fadhili zake zote. Akusamehe maovu yako yote, Akuponya magonjwa yako yote, Aukomboa uhai wako na kaburi, Akutia taji ya fadhili na rehema, Aushibisha mema uzee wako, Ujana wako ukarejezwa kama tai, Isaya 38:16-17 Ee Bwana kwa mambo hayo watu hu